Katika episode ya pili ya mfululizo huu, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano TANAPA, Catherine Mbena anaelezea kwa kina kazi mbalimbali zinazofanywa na Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) katika kuhakikisha maliasili zilizopo ndani ya hifadhi za Taifa zinaendelea kulindwa na kuhifadhiwa kwa faida ya kizazi hiki na vizazi vijavyo.