Naamini watu wengi wameshasikia juu ya kile kinachojulikana kama Mpango Mpya wa Ulimwengu (New World Order). Hata hivyo, wapo pia wengine wengi ambao hawana habari juu ya kile kinachoendelea kuhusiana na mpango huu.
Mpango Mpya wa Ulimwengu ni mpango wenye nia ya kuusuka ulimwengu upya ili uweze kuwa tofauti na ulivyo sasa; ili uweze kuendana na malengo ya hao wanaoutaka. Mpango huu ni mkakati kabambe unaosimamiwa na watu wenye nguvu duniani, yaani wenye nguvu za kiuchumi, kisiasa, na hata kiroho.
Malengo ya mpango huu ni mengi. Kati yake ni haya yafuatayo: