Mchungaji Mmasa na Mwalimu Mike tunafundisha Biblia katika masomo ya siku kwa Jumapili ijayo ili kuwasaidia watu wote na hasa watumishi katika maandilizi yao.
Wiki hii ya Jumapili tarehe 24/3 ni Jumapili ya Mitende, ukurasa 93 katika kitabu cha sala.
Kwenye hiyo sehemu ya kwanza tunafundisha juu ya tukio la Yesu kuingia Yerusalemu kwa shangwe katika Marko 11:1–10 na tunafafanua mawazo kadhaa katika somo la Injili ambalo ni Marko 14:32–15:41.
Sehemu ya pili, podi ifuatayo, inahusu Wazo Kuu la siku, Njia ya Msalaba, na masomo mengine, 1 Wakorintho 1:18–25, Zaburi 22, na Isaya 50:4–9.
Karibu!