Listen

Description

Kaa tayari kusikiliza mazungumzo mazuri, yenye kufurahisha, kufundisha na kujenga kwenye episode yetu ya 78.

Michael Baruti, na mgeni wetu maalum wa siku ya leo, mtangazaji mashuhuri bwana Harris Kapiga wanazungumza kuhusu dunia ya “u-baba”, na ina maana gani kwa mtoto wa kiume. 

Na ndiyo sababu ya mazungumzo ya leo kuitwa “Baba na mtoto wa kiume”. 

 

Ni kazi gani ambayo baba inabidi afanye ili aweze kulea mtoto wake wa kiume katika dunia ya sasa?.

Katika maongezi haya Michael na Harris Kapiga ambaye ni baba wa watoto watatu wa kiume wanazungumza na ku-“share” uzoefu wao, busara, ushauri, mafaniko, changamoto, maanguko na upekee wa safari walizopitia na wanazoendelea kupitia wakiwa kama watoto wa kiume, lakini pia wakiwa kama wakina baba wanaolea watoto katika dunia ya sasa yenye mambo mengi sana.

  

Fanya ku-subscribe kwenye ukurasa wetu wa “YouTube” na usikilize na kufurahia mazungumzo haya. 

 

Ni mazungumzo muhimu sana kwa kina baba wote, hususani wale wanaolea watoto wa kiume