18 Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu, Naam, kuna manne nisiyoyafahamu.
Mithali 30:18
19 Mwendo wa tai katika hewa; Na mwendo wa nyoka juu ya mwamba; Mwendo wa merikebu katikati ya bahari; Na mwendo wa mtu pamoja na msichana.
Mithali 30:19
20 Hivyo ndivyo mwendo wa mwanamke mzinifu; Hula, akapangusa kinywa chake, Akasema, Sikufanya uovu.
Mithali 30:20
21 Kwa ajili ya mambo matatu nchi hutetemeka, Naam, kwa ajili ya manne haiwezi kuvumilia.
Mithali 30:21
22 Mtumwa apatapo kuwa mfalme; Mpumbavu ashibapo chakula;
Mithali 30:22
23 Mwanamke mwenye kuchukiza aolewapo; Na mjakazi aliye mrithi wa bibi yake.
Mithali 30:23
24 Kuna viumbe vinne duniani vilivyo vidogo; Lakini vina akili nyingi sana.
Mithali 30:24
25 Chungu ni watu wasio na nguvu; Lakini hujiwekea chakula wakati wa hari.
Mithali 30:25
26 Wibari ni watu dhaifu; Lakini hujifanyia nyumba katika miamba.
Mithali 30:26
27 Nzige hawana mfalme; Lakini huenda wote pamoja vikosi vikosi.
Mithali 30:27
28 Mjusi hushika kwa mikono yake; Lakini yumo majumbani mwa wafalme.
Mithali 30:28
29 Kuna watatu wenye mwendo wa kupendeza, Naam, wanne walio na mwendo mzuri.
Mithali 30:29
30 Simba aliye hodari kupita wanyama wote; Wala hajiepushi na aliye yote;
Mithali 30:30
31 Jimbi aendaye tambo; na beberu; Na mfalme ambaye haasiki.
Mithali 30:31
32 Ikiwa umefanya kipumbavu kwa kujikuza; Au ikiwa umewaza mabaya; Basi weka mkono wako juu ya kinywa chako.
Mithali 30:32