Look for any podcast host, guest or anyone
Showing episodes and shows of

Salama Na

Shows

Adrián Salama ¡Sin Censura!Adrián Salama ¡Sin Censura!El ÚLTIMO Video de Adrián SALAMA ❗️¿Ya no habrán MÁS EN VIVOS? | Nos vemos pronto👉 CONOCE MÁS DE LO QUE HACE ADRIÁN: https://www.salamapedia.comHoy quiero platicar con ustedes...#preguntas #podcast #adriansalama ✅ EN VIVO DE LUNES A JUEVES A LAS 7PM HORARIO CDMX @AdrianSalama #nosmamaelchisme y usamos el chisme educativo para poder llevar a las personas más acceso a la salud mental. Reaccionamos a lo más VISTO de youtube para poder así generar conciencia y diversión. Creamos #podcast de #psicologia para generar más conciencia sobre los daños que existen cuando no hay buena #saludmental ✅ ¿Q...2025-01-311h 02Adrián Salama ¡Sin Censura!Adrián Salama ¡Sin Censura!CANCELADO❗️ El "Psicólogo" MÁS OD1ADO de México | Dr. Salama REACCIONA a ADRIÁN MARCELO#nosmamaelchisme El iceberg de #adrianmarcelo. Aléjense de alguien como él.🔥APRENDE CON MIS CURSOS ONLINE:Acaba con tu ansiedad dando click aquí ❗️✨https://www.adriansalama.comTen la relación de pareja que siempre soñaste 💕https://www.adriansalama.com Usamos el chisme educativo para poder llevar a las personas más acceso a la salud mental. Reaccionamos a lo más VISTO de youtube para poder así generar conciencia y diversión.✅ Adquiere AHORA mi nuevo curso online "Toma el control de tu ansiedad" AQUÍ ⬇︎ ht...2024-08-221h 21Adrián Salama ¡Sin Censura!Adrián Salama ¡Sin Censura!🚨Las CONSECUENCIAS de consumir NOPOR explicadas PSICOLÓGICAMENTE | #SinCensura por Adrian SalamaMis Salamandras! Hoy tenemos esta nueva sección llamada Sin Censura donde hablaremos de temas que DESAFÍAN LA MENTE.Hoy tocaremos las consecuencias psicológicas del consumo de la nopor tanto en hombres como mujeres.¿De qué otra cosa les gustaría que habláramos?🚨🚨INSCRÍBETE AQUÍ AL CURSO DE PAREJAS 100% ONLINE: 🚨🚨https://www.adriansalama.com/cursos-online✅ EN VIVO DE LUNES A JUEVES A LAS 7PM HORARIO CDMX @AdrianSalama  #nosmamaelchisme y usamos el chisme educativo para poder llevar a las personas más acceso a la...2024-04-0325 minAdrián Salama ¡Sin Censura!Adrián Salama ¡Sin Censura!ADRIAN SALAMA reacciona a Psicóloga Explica el PERFIL de un AS3S1N0El podcast original se llama: Psicóloga Forense "Los perfiles psicológicos de los Asesinos" Dra. Rocío López | pepe&chema podcast🚨🚨INSCRÍBETE AQUÍ AL CURSO DE PAREJAS 100% ONLINE: 🚨🚨https://www.adriansalama.com/cursos-online✅ EN VIVO DE LUNES A JUEVES A LAS 7PM HORARIO CDMX @AdrianSalama  #nosmamaelchisme y usamos el chisme educativo para poder llevar a las personas más acceso a la salud mental. Reaccionamos a lo más VISTO de youtube para poder así generar conciencia y diversión. Creamos #podcast de #psicologia para generar más concienci...2024-03-191h 31Adrián Salama ¡Sin Censura!Adrián Salama ¡Sin Censura!Adrian Salama REACCIONA a Sebastián Yatra ¿IRRESPONSABLE EMOCIONAL? Canta sobre AMOR y NO cree en el¿Canta sobre el amor pero no cree en el?Vicky Martín Berrocal estrena nueva temporada de ‘A solas con’ en Podium Podcast con las confidencias de Sebastián Yatra. Grabado en el Four Seasons Hotel Madrid, el cantante, actor y modelo colombiano habla a corazón abierto sobre su vida. Desde su primer enamoramiento a sus dos únicas novias, del rol fundamental de su madre en su carrera, de los momentos estelares, de los complicados, de sus valores o del sexo, entre otras confesiones.‘A solas con Vicky Martín Berrocal’ es el podcast don...2024-02-232h 10Salama NaSalama NaSE7EP38 - SALAMA NA MFAUMEX2 | TOE - TO - TOEMfaume Mfaume ni yule mwana ambaye akitokea sehemu ni sahihi kwako kuwaambia wahusika kwamba jamani, mwamba huyu hapa! Muonekano wake pekee unamfanya mtu ajue yuko kwenye presence na mtu maalum na baadae ukishajua hasa nini anafanya basi huwezi ku doubt yote ambayo utaambiwa juu yake lakini kubwa zaidi ukipata sasa nafasi ya kumuona anapokua kazini kwake hapo ndo utakaposhia kumpa nyota zake zote anazostahili kama bondia. Tena popote pale, iwe akiwa gym au ulingoni ambapo kadhaa washachezea shurba kutoka kwake. Mfaume ni kama wengi wetu ambao tumetokea katika familia za kawaida tu ambayo malengo ya wazazi wetu...2023-03-0259 minSalama NaSalama NaSE7EP37 - SALAMA NA TOUFIQ | Um'PENDAEToufiq ni moja ya majina makubwa kati ya wafanya biashara wazuri na sasa mwanasiasa na Mbunge wa Mpendae, kwa wazee na vijana wa visiwani humo yeye ni mmoja wa mifano ya kuigwa ingawa kwake yeye yaliyo mengi kwenye maisha yake ni nguvu kubwa ilifanywa na Marehemu Mzee wake Ndugu Salih Hassan Abdullah Turky aka Mr White ambaye na yeye akiacha ukweli kwamba alikua tajiri na mfanya biashara nzuri huko visiwani ila yeye pia alikua kipenzi cha wananchi wa Jimbo la Mpendae ambapo sasa Toufiq ndo anaye liongoza jimbo hilo baada ya Mzee wake kutangulia mbele ya haki. Mwenyezi Mungu...2023-02-2335 minSalama NaSalama NaSE7EP36 - SALAMA NA ALLY BEE | KULE NI KULE…Kwenye jiji la ‘Maraha’ hapa nyumbani kwetu Tanzania ambayo kwa miaka ya hivi karibuni sehemu za starehe zimekua tele na kila mmoja ana uwezo wa kula bata zake vizuri tu kulingana na urefu wa mfuko wake basi hakuna ambaye HAJUI jina la DJ huyu mahiri ambaye kwa ubunifu wake ameweza sana kubadilisha kabisa jinsi ambavyo wenzake walomtangulia walikua wanafanya. Yaani Ally alikichukua kitabu cha jinsi ya kutoa burudani kama DJ na kukichanachana na kisha akaanza kuandika cha kwake, ambacho mpaka tunaenda mtamboni kiiila msomaji wake anapeeenda ambayo yameandikwa na ambayo anaendelea kuyaandika. Wakati msimu huu unaanza Ally Bee...2023-02-161h 04Salama NaSalama NaSE7EP35 - SALAMA NA EVANS BUKUKU | STICK - TO- ITIVENESSUlikua muda mwingi hasa umepita toka mara ya mwisho nilionana na Evans wa Bukuku na kukaa naye chini kisha tukaongea. Na ki ukweli hajawahi kuwa rafiki yangu wa karibu ila ni mtu ambaye tunafahamina na kuheshimiana. Hustle zake nazifahamu kwa ukaribu maana industry ambayo tunafanya kazi ndo hiyo hiyo kwahiyo nikama chakula, tusipokutana jikoni basi tutakutana kwenye sahani. Kama ilivyo kwa watu wengi nimekua nikimsikia kwenye radio mbali mbali katika safari yake kama mtangazaji wa vipindi mbalimbali lakini pia nimekua nikimuona kwenye majukwaa mbalimbali akifanya shughuli zake za ku host sherehe au matamasha kadhaa. Kwenye kitabu changu...2023-02-091h 13Salama NaSalama NaSE7EP34 - SALAMA NA FETTY DENSA | KUTOKA UBAVUNI...Kwa ambao wanafuatilia mpira hapa nyumbani wanamjua mchezaji huyu mahiri wa Simba Queens lakini ambao wanafuatilla soka la wanawake hawa watakua wanaelewa uwezo binafsi na uhodari wake wa kucheza namba tofauti tofauti uwanjani ila ukimkuta kaikamata mbavu ya kulia aidha kwa Simba au timu ya Taifa ya Tanzania. Fatuma Issa ni mtu na nusu, hakuna mpenzi wa mpira au kocha yoyote wa mpira anaweza akamuacha kwenye benchi wakati team inatafuta matokeo au inataka kuwaonyesha walofika kuwaangalia vipaji ambavyo wanavyo kwenye kikosi chao. Kwa yoyote yule na kwa vyovyote vile, Fetty Densa, ni lazima AANZE. Ananikumbusha sana mimi...2023-02-021h 12Salama NaSalama NaSE7EP32 - SALAMA NA MRISHO NGASSA | MACHACHARI…Mrisho Halfani Ngassa alikua top top top footballer na kwa bahati nzuri nishawahi kumshuhudia akiwa kazini kwake, tena ukimkuta kaamka vizuri basi uhakika wa burudani ni UHAKIKA . Na kipindi ambacho alikua kwenye peak yake pia kulikua na vitasa imara na magolkipa wazuri tu lakini nna uhakika kila mmoja kati yao ana la kusema kuhusu winga na forward hii machachari ambayo nchi yetu ishawahi kuona. Hakuna kitasa ambacho hakijawahi kukataa kufungua mlango muda ambao Mrisho Ngassa alikua anakuja kupiga hodi. Uzuri wake alianza kucheza mapema sana na kwasababu alikua machachari basi hata utulivu kidogo wakati anakua ulikua sio...2023-01-191h 20Salama NaSalama NaSE7EP31 - SALAMA NA KUSAH | NG’WANA AZAIZA!!Kutoka zake Lushoto huku mkoani Tanga ni kijana mtanashati ambaye anajua kama amekuja town au jijini Dar es Salaam kwasababu ya kusaka pesa ili abadilishe maisha yake na ya wale ambao wamemzunguka. Na kila alikumbuka ambapo ametoka basi spidi ya kuhakikisha kalamu yake haivuji na inaandika kwa muandiko mzuri ili kila ambaye atabahatika kusoma kile ambacho yeye kakiwaza na kukiandika basi azame kwenye dimbwi lake na endelee kumsikiliza mpaka pale yeye mambo yake yatakapoenda, na kwa story ambazo amenipa basi ukinasa kwenye kitabu chake itakuia vigumu kutoka kwasababu amepanga kuwepo kwa muda mrefu sana, nia na madhumuni yake ni...2023-01-1250 minSalama NaSalama NaSE7EP30 - SALAMA NA BRENDA | MY DEAR…Ushawahi kumuangalia mtu kwa mbali na kujiuliza maswali mengi juu yake? Maswali kama siku yake ikoje, amewezaje? Kama ana familia? Ki kawaida huwa anaamka saa ngapi? Amesoma wapi? Siku yake anaipangaje? Ana watoto? Mtoto? Huwa anawaandaa kwenda shule? Muda je wa kukaa nao? Elimu yake ameipatia wapi? Kwenye familia aliyotoka je? Wazazi wake wapo? Na je wanajivunia yeye kwa kiasi gani? Sasa ili kupata majibu ya maswali hayo yote ilibidi tumtafute Bi Brenda Msangi-Kinemo ambaye ndo nilikua namzungumzia hapo juu. Kama wewe utakua mtu wa kujua ambayo yanaendelea nchini, na pia kama ni mkazi wa Dar es...2023-01-051h 06Salama NaSalama NaSE7EP29 - SALAMA NA DEO GRATIUS | PRIVILEGED?! Deo Gratias, jina tu linatosha kujielezea kama wewe nawe utakua kama mimi wa kutaka kujua maana ya majina ya watu ili uweze kujua tabia zao au ujiulize wazee wake walikua wanafikiria nini wakati wanaamua kumpa jina hilo mtoto wao. Kwa Deo maana imejibeba na imejikamilisha na kwa yeye kuamua kubaki na jina lake hilo hilo mpaka kwenye stage ambako ndo sehemu yake ya kazi inabidi hilo nalo likuambie jambo kuhusu yeye na jinsi ambavyo anajichukulia na kuyachukulia mambo ambayo ameyachagua kuyafanya. Shukrani ziende kwa Mungu ndo maana ya jina lake, shukrani ziende kwa Mungu kwa kila alifanyalo l...2022-12-291h 11Salama NaSalama NaSE7EP28 - SALAMA NA GARA B | BABA SHUGHULIJina MC Gara B ni miungoni mwa majina makubwa sana kwenye ulimwengu wa kazi ambayo mwenzetu huyu amechagua kuifanya. Familia yake, mke na watoto, wazazi wake na wa mkewe pengine, Ndugu jamaa na marafiki na waajiriwa wake wanakula vizuri kwasababu ya kipaji chake Ndugu yetu huyu. Ni mwanaume ambaye akiwa kazini kwake furaha na burudani ambayo huwapa wateja wake ndo inayomfanya azidi kuenda mbali kwenye tasnia hiyo ya ushereheshaji. Again, yeye ni mmoja ya BORA kadhaa ambao wanafanya kazi kama yake. Mtandao wa kijamii ni kitu kimoja chenye nguvu sana kwenye miaka ya hivi karibuni, kwa ushahidi...2022-12-221h 00Salama NaSalama NaSE7EP27 - SALAMA NA BARAKA KIZUGUTO | NEUTRALBaraka Kizuguto si moja ya majina yajulikanayo miungoni mwa wa Tanzania wengi ambao asilimia kubwa ya wenye simu za mkononi hupendelea zaidi habari za maisha ya watu maarufu na mashuhuri, kutaka kujua wanakula nini, wanaishi wapi, wanalala wapi, wanalala na nani na kadhalika. Na kama wewe ni mmoja wa watu hao na si mpenzi wa mpira basi kumfahamu mgeni wetu wa kwenye kiti chakavu wiki hii itakuwia vigumu. Ila kwa wale watu wa mpira, au wafanyakazi kwenye Vyama vya mpira hapa kwetu na Afrika kwa ujumla au wachezaji au waalimu wa mpira jina na sura yake si ngeni kabisa...2022-12-151h 12Salama NaSalama NaSE7EP26 - SALAMA NA MASOUD KIPANYA | HERI KUFA MACHO…Habibi Masoud Kipanya ni Ally Masoud Nyomwa ambaye ni LEGEND. Kwa mujibu wake alizaliwa huku kakunja ngumi na dhana yake ni kwamba alizaliwa ili awe bondia! Kwa anacho kifanya na ambacho amekua akikifanya tena kwa ufasaha kwa miaka nenda miaka rudi bila ya shaka ni UBONDIA. Hakuna ambaye atabisha juu ya hilo. Amekua akipigania mambo tele na kuyasemea mengi pamoja na kuchekesha na kuelimisha kupitia kalamu yake. Kwa mujibu wake yeye ni mbobevu katika taaluma ya kupuuza na kuchukulia mambo poa kwa kipindi sasa. Lakini pia anaamini yeye ni MTATA. Tukienda mbele na kurudi nyuma, hapo kwenye UTATA hakuna...2022-12-081h 51Salama NaSalama NaSE7EP24 - SALAMA NA LULU DIVA | UKIPATA KINYAKUEKuna mambo mengi wakati mwengine ambayo yanakua yanaendelea au yalitokea kwenye maisha ya baadhi ya watu ambao huja kukaa kwenye kiti chetu chakavu na meza yenye kigae. Ila kwasababu zilizo wazi za kuwataka wasijisikie uncomfortable na pengine kuwafanya hata ambao wangependa au ambao tungependa waje nao wasijiskie hivyo ndo kanuni ambayo tumeamua au niseme niliamua kipindi huko nyuma kuifuata. Nia na madhumuni ya session zetu hizi zaidi ni kuwapa watu maua yao wakiwa hai, sisi nasi kuskiliza hadithi za maisha yao ambazo zitatupeleka sehemu fulani katika maisha yatu na hili pia humuambia kila mgeni anapokalia tu kiti chetu chakavu...2022-11-301h 15Salama NaSalama NaSE7EP25 - SALAMA NA DORIS MOLLEL | HALF WOMAN, HALF AMAZINGDoris Mollel kwa kuanzia tu tuanze na jina lake, ni zuri lenye kukumbukwa ki rahisi, yeye mwenyewe pia ni mrembo na mkarimu, sana. Roho yake ni kama rangi yake, nyeupe na kwa bahati Mimi namfahamu yeye kiasi kwa kupitia rafiki zangu ambao yeye anafanya nao kazi na pia ana mahusiano nao mazuri, sana. Pia namfahamu mume wake ambaye tukianza shindano la kumtafuta nani mkarimu kati yao tunaweza kukamaliza kwa suluhu. Huwa naamini Mwenyezi aliwakutanisha ili kwa pamoja waweze kufanya makubwa kwaajili yao na familia zao na jamii ambayo imewanzunguka ambayo kwa kiasi kikubwa ina uhitaji wa yale ambayo wao...2022-11-241h 15Salama NaSalama NaSE7EP22 - SALAMA NA ANNA TIBAIJUKA | LA PROFESSEURNilipoandikiwa ujumbe mfupi na Edwin Bruno ambaye ni mkwe wa Professor kwamba Mama amekubalia kufanya kipindi na sisi siku hiyo ya Jumapili akishatoka church nilihisi kama naota. Mwenyezi Mungu anajua kwa kiasi gani tumekua tukitaka kufanya maongezi nae kwenye kipindi chetu. U busy wake na pengine mara nyingi kutokuwepo Dar es Salaam napo palikua panaleta ugumu, nyengine ilkua ni tarehe zetu za kufanya production na availability yake zilikua zinapishana sana. So unaweza ukaelewa excitement ambayo nilikua nayo baada ya finally samaki kujaa kwenye ndoana. Professor Anna Tibaijuka ni LEGEND miongoni ma magwiji kwenye nchi hii kwa kazi...2022-11-101h 01Salama NaSalama NaSE7EP21 - SALAMA NA BILLNASS | MJUKUUKatika pita pita zangu siku si nyingi nilimsikia mtu akimzungumzia mgeni watu wa wiki hii kwamba ni ‘Jay Z’ wa Bongo na si kwasababu kamuoa mmoja wa wasanii hodari wa kike na ambao wako juu ki muziki, ila pia akili yake ya kibiashara kwa kiasi kikubwa imemfanya yeye aone hivyo. Kwa ufahamu wangu niliambiwa na kushuhudia suala la maneno na mawazo ‘kuumba’. Pale mtu au watu wanapo kuona na ukichanganya na juhudi zako na nia na madhumuni ya wewe kutaka kufika pale basi mengine kutimia huwa ni suala la wakati tu. Hivyo pia ndivyo ambavyo mimi namuona Ndugu Wi...2022-11-031h 15Salama NaSalama NaSE7EP20 - SALAMA NA CAROL NDOSI | ANAMEREMETAUshawahi kuwa na mtu ambaye mnafahamiana vizuri miaka nenda na miaka rudi na hata pengine kwa u busy wa maisha zikapita siku hamjaongea lakini unajua yuko sawa yeye na Familia yake na mambo yanaenda vizuri, na kama isingekua hivyo basi ungekua ushajua? Ambaye unajua kukiwa na situation flani basi yeye anatafanya jambo flani na kuzima au kuwasha moto, na kama kuna neno umeambiwa kasema unajua kabisa ni kweli au si kweli? Au kama una suala unataka kulifahamu vizuri linalohusu mambo fulani na jibu ambalo atakupa yeye ni la 100 na hatapindisha hata kidogo? Basi huyo ni Carol Moses Ndosi kwa...2022-10-271h 05Salama NaSalama NaSE7EP19 - SALAMA NA DITTO | TUNERLameck Ditto Sr ni Baba, Mwalimu, mwanamuziki, muandishi, mentor, mume na zaidi ya yote ni mwana tu ambaye maisha alopitoa kipindi anakua hayajawahi na wala hayatawahi kumsahaulisha yeye ni nani na wapi ambapo ametokea na wapi anataka sana kuelekea maana huko ndo kwenye kesho yake, na kwa kumsikiliza ambavyo nimemsikiliza, kesho yake anaithamini sana na amekua akiiandaa vizuri ili hata siku moja asije akakwama na kuanza kuishi maisha ya jana ambayo yalikua si mazuri hata kidogo. Yeye na Baba yake mzazi walikutana kwa ‘bahati mbaya’ tunaweza tukasema hivyo maana wakati yuko zake Morogoro akiendelea na maisha ya kuis...2022-10-201h 20Salama NaSalama NaSE7EP18 - SALAMA NA FAROUK KAREEM | SAILORHii nayo ni moja ya zile ambazo ziliuliziwa sana na kwa muda mrefu nasi kwa upande wetu tumekua tukiifukuzia tuweze kukaa na mwamba huyu hodari kutoka Zanzibar. Mimi mwenyewe ambaye nimekua nikifanya kazi kwenye kiwanda hiki cha burudani nilikua na hamu ya siku moja kuwa kwenye meza moja na Ndugu yangu huyu, kuweza kumtazama usoni na kumuuliza yote ambayo nilikua nataka kumuuliza kwa kipindi kirefu sana. Maana hata mimi nimekua nikimsikiliza miaka nenda miaka rudi na siku zote emeemdelea kutuhabarisha kwa sauti ile ile na spidi ile ile. Ukiskia mtu ameweza kuwa bora toka siku ya kwanza basi moja...2022-10-131h 23Salama NaSalama NaSE7EP17 - SALAMA NA ROSE MUHANDO | NIPE UVUMILIVUKatika binadamu ambao walinipa wakati mgumu na kusubiri kwingi kabla ya kuja kukaa kwenye meza yetu ya kigae na kiti chakavu basi mmoja wao ni Rose huyu wa Muhando. Upatikanaji wake ni kama ukitaka kumuona SIMBA mbugani, lazima uamke asubuhi na mapema au uwe na bahati ya mtende kama ambayo sisi tumepata. Ingawa tulisubiri kwa masiku tele na miezi tele katikati ya mwaka huu tuliweza kumpata na kukaa nae chini ili tuweze kuzungumza nae. Rose ni wa moto sana, kalenda yake imejaa safari tele za nje na ndani ya nchi, anazunguka mara kwa mara kwaajili ya kutoa...2022-10-061h 20Salama NaSalama NaSE7EP16 - SALAMA NA ZAHIR ZORRO | KIMULIMULIZahir Ally Zorro ni mkongwe wa muziki wa dansi na kwa habari ambazo nimepata ni kwamba enzi zake alikua wa moooto sana tena kwenye kila nyanja, kuimba, kuandika, kupiga gitaa na mpaka uvaaji, alikua handsome boy sana na ulimbo kwa kina Dada enzi hizo. Utashi na ucheshi na u sharp wake ndo ambao ulikua unamfanya asimame PEKEE kwenye kadamnasi ya wanamuziki wengi wa kipindi hiko. Naomba nikukumbushe pia kwamba enzi hizo zilikua pia si za kuzichukulia poa kabisa, maana ushindani wa bendi na vipaji binafsi ulikua wa hali ya juu sana, na yeye kama yeye alikua moja ya wale...2022-09-3051 minSalama NaSalama NaSE7EP15 - SALAMA NA MCHUNGAJI RICH BILIONEA | SERMONKipindi cha nyuma kidogo nilifanya lile ambalo huwa nafanya la kuwashirikisha rafiki zangu na team kuhusu list ya watu ambao wangependa kuwaona kwenye kiti chetu chakavu na sababu za kwanini hasa waje kwenye meza ile yenye kigae kwa juu maana tukisema tutaje majina tu bila ya sababu thabit za wao kuja pale tunaweza tukaondoa maana yenyewe ya kuwa na watu wenye story za kuvutia na kutufunza kama ambavyo tumekua tukifanya. Jina la mgeni wetu huyu lililetwa kwangu na Michael (Mx) Mlingwa na Ndugu yangu Elbogast Myaluko ndo alinipatia mawasiliano naye na kuanzia hapo mengine yamebaki kukhadithiwa kama hivi. 2022-09-221h 05Salama NaSalama NaSE7EP14 - SALAMA NA COACH EVARIST | FIRST QUARTEREvarist Mapunda ni moja wa makocha wangu wa maisha haya ninayoishi sasa hivi, ananifahamu toka nikiwa na miaka 17 mpaka sasa hivi ingawa hapa katikati baada ya ‘kuwa mkubwa’ nilipoteana nae kwenye mahangaiko ya kujitafuta na kutafuta maisha. Ila Mimi na yeye tunajua kila mmoja wetu ni mtu wa aina gani na anamaanisha NINI kwa mwengine. Ukiwauliza watoto na wakubwa wengi wa Upanga watakuambia nini yeye pia anamaanisha kwenye maisha yao, lazima atakua na simulizi kuhusu mwalimu huyu hodari wa basketball na maisha, kama hadithi hiyo itakua haimhusu yeye directly badi itakua inamhusu Ndugu yake au mtoto wake au h...2022-09-151h 19Salama NaSalama NaSE7EP13 - SALAMA NA MARDHIYA | HIARI…Salum Mardhiya ni mmoja ya watu maarufu sana kwenye visiwa vya marashi ya karafuu yaani kule kwetu Zanzibar. Ni mmoja ya waalimu hodari anayeongoza kwa kutoa Da’wa kwa watu ambao wanasumbuliwa na matatizo mbali mbali. Kwenye nyumba karibu zote wanamfahamu maana huonekana mara kwa mara kwenye maeneo mbali mbali ili kusaidia wale ambao wanahitaji kisomo chake. Binafsi nilifahamiana nae kupitia rafiki ambae alinitambulisha kwake mapema mwaka huu, tena haikua imepangwa wala, alikuja sehemu ambayo mie nilikuwepo kuja kupata chai na mimi bahati nzuri nilikua maeneo hayo so mtu akatutambulisha, na akaambiwa kama Mama yangu ni mgonjwa yuko hospitali na...2022-09-0850 minSalama NaSalama NaSE7EP12- SALAMA NA DR TULIA | BULYAGA 1976Tulia Ackson ni jina kubwa kati ya majina makubwa kwenye Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na kwa sisi kuweza kulipata jina kubwa na kukubali kuja kuketi kwenye kiti chetu chakavu ilikua ni BARAKA sana. Ila ukiachana na kwamba ni jina kubwa ila yeye ni binadamu, tena wa kawaida tu. Ni Mama, ni mke, ni Dada, ni Binti kwa Mama yake na ni Mbunge kwa wana Mbeya mjini lakini pia ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wadhifa ambao baada ya uchaguzi wa 2020 alirudi bungeni kama Naibu Spika ila baada ya aliyekua Spika kujiuzulu Dr...2022-09-0151 minSalama NaSalama NaSE7EP11 - SALAMA NA MARTIN KADINDA | PLEASANTMartin Kadinda ni rafiki yangu, ni moja ya wale wana ambao hana makuu na zaidi yeye anapeeenda sana kucheka, hata ukiangalia picha zake yeye ana tabasamu tu. Pengine hiyo ndo siri ya mafanikio yake tofauti yake na wengine na pengine hiyo ndo sababu ya mimi kumpenda sana. Pia ni FUNDI, tena mzuri tu sana. Kati ya mafundi wachache WAKWELI wa nchi hii Martin ni mmoja wapo, kama hawezi hawezi, hata siku moja hawezi chukua kazi yako alafu siku ya siku akakuharibia shughuli au mtoko. Kama yuko busy na mambo yake atakuambia rafiki, hiyo sitoweza tafadhali mtafute mtu mwengine aifanye...2022-08-251h 02Salama NaSalama NaSE7EP10 - SALAMA NA DR CHENI | SUKAGrowing up kwenye mitaa ya Dar es Salaam na TV stations kali wakati huo zilikua na presenters makini na vijana ambao kwa kiasi kikubwa waliifanya tasnia hiyo ipendeze sana. Kuanzia vipindi vya watoto, vya muziki, filamu kutoka nje na tamthilia kutoka nje pia zilikua tamu sana, ukianza kuangalia TV kuanzia jioni hakuna mtu alikua anabanduka mpaka saa nne au tano za usiku, na kama ulikua jobless kama mimi enzi hizo basi ulikua unaunganisha na kuangalia marudio ya vipindi vya muziki ambavyo tayari ulikua ushaviona jioni yake, ila kwasababu ya utamu wake na ku enjoy kile unaona kurudia ilikua easy...2022-08-181h 16Salama NaSalama NaSE7EP08 - SALAMA NA SAMATTA | HEADMASTERKila kijana wa ki Tanzania ambae anaupenda na kuuthamini mpira wa miguu na ambaye angependa ndo iwe kazi ya maisha yake basi Mbwana Ally Samatta ndiye role model wake, hakuna doubt kwamba watakua na mapenzi na Cristiano Ronaldo au Leo Messi au Kylian Mbappe au Marcus Rashford ila yule ambaye amewaaminisha kwamba INAWEZEKANA ukacheza POPOTE hapa duniani na hasa kwenye ligi yetu pendwa ya Uingereza ni Samatta. Rafiki tu kutoka Mbagala rangi tatu ambaye kashacheza saaana ndondo na makombe ya mbuzi wakati anakua na mwisho wa siku akaenda kucheza kwa wazungu na bado anaendelea kutafuta rizki yake huko, hata...2022-08-041h 00Salama NaSalama NaSE7EP07 - SALAMA NA DR KUMBUKA | YAANI…Dr Kumbuka ni influencer mkubwa kwenye masuala ya mahusiano na maelewano inapokuja kwenye suala zima la ushauri na mashauri kwa watu wengi ambao wamekua wakimsikiliza na ambao wanamsikiliza kila siku za wiki anapokua kwenye kipindi cha Uhondo pale EFM. Na yeye kuwa pale hakufika kwa bahati mbaya. Ila pengine alipo anzia kazi yake pale Times FM ndo ilikua kama bahati kufika. Anakumbuka jinsi ambavyo alikua zake tu mtaani wakati mtangazaji wa Times FM wakati huo Bi Dida Shaibu alipokua mtaani akitafuta watu wenye kipaji cha ‘kuchamba’ watu wengine. Anasema wanawake ndo walikua wametawala jukwaa huku wakishusha maneno mengi ya kara...2022-07-281h 07Salama NaSalama NaSE7EP06 - SALAMA NA MTANI | SO SILKYUshawahi kukutana na wale watu ambao wao ni wa pole tu sana na wanajipenda tu sana ila hawana tu muda wa kuringa au kuji mwabafy kwasababu wao wako talented au wana kipawa kutoka kwa Allah na wanajua? Well mi nishawahi kukutana na watu kama hao na mmoja wao ni mgeni wetu RASMI wa wiki hii ya episode ya sita ya SalamaNa msimu huu. Anaongea kwa utaratibu na kujua kile atakacho, anakipataje na akisha kipata atafanya nacho nini. Huyo sasa ndo mwanangu Mtani Nyamakababi, aka Mtani Beskope. Kijana wa ki Tanzania mwenye kuelewa somo la leo na ukiachana...2022-07-2155 minSalama NaSalama NaSE7EP05 - SALAMA NA OSCAR OSCAR | UALIMU?! SI WITO!!Mwaka 2018 ndo nilimfahamu Oscar baada ya kukutana nae kwenye kituo changu cha kazi ya kutangaza mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika jijini Johannesburg nchini Afrika ya Kusini. Alikua mmoja ya watu ambao walinikaribisha vizuri sana kwenye team na kwa wakati huo yeye ndo alikua anaishikilia rekodi ya kuwa ndo mtangazaji mdogo zaidi kwenye team ya watangazaji nami nikaja kama Binti PEKEE ambaye ambaye alikua anatangaza mpira wa miguu kwa lugha ya Kiswahili. Combination yetu ilikua nzuri sana na kwa kipindi hiko ambacho kilikua cha mwezi mmoja tulielewana na ku bond vizuri sana. Oscar anapenda raha, anapenda...2022-07-141h 11Salama NaSalama NaSE7EP04 - SALAMA NA SHEIKH KIPOZEO | شيخSheikh Hilali Shaweji Makarani au Sheikh Kipozeo ni mtu wa watu, au niseme kama ambavyo tunasema kwetu Uswazi, Sheikh ni mwana wa wana, anaweza kuwapa wana darsa kwa lugha yao na wakawa huru na wao kusema maoni yao au uelewa wao kwa raha na bashasha nyingi na naamini hii imemfanya yeye awe ni mmoja ya Ma Sheikh wanao tambulika zaidi kwenye mitandao ya kijamii nje na ndani ya Tanzania. Lugha hiyo ya wana ambayo anaitumia inasaidia sana kufikisha ujumbe ambao ameukusudia kwa wakati huo na ikapata mpaka majadilioano, majadiliano hayo ndo huzaa majibu ya maswali mengi ambayo wengi hujiuliza.2022-07-0758 minSalama NaSalama NaSE7EP03 - Salama Na Quick Rocka | SWITCHERAbbot Charles ni jina maarufu kwa wanaoijua historia na wana zuoni, pengine umaarufu wa jina ndo sababu ya Baba yake kuamua kumpa mtoto wake wa kiume akitegemea na kijana wake atakua na ukubwa huo kwa lolote ambalo ataamua kufanya kwenye maisha yake, unaujua ule usemi kwa kiswahili kwamba maneno huumba? Mwenzangu, hata majina huumba, tena sana tu kwahiyo wakati mwengine utakapokua unafikiria jina la mwanao ni vyema kujiridhisha kwanza, unafanya kazi flani ya kipolisi ya kuchunguza ili mwanao asije akawa mtu fulani asiye na dira. Quick Rocka aka Switcher aka Baba aka Kaka Fule ni mdogo wangu...2022-07-011h 05Salama NaSalama NaSE7EP02 - Salama Na Engineer Hersi | A BREATH OF FRESH AIR Kama kichwa cha habari kinavyosema, Engineer Hersi ndo chachu ya furaha kwa mashabiki wa moja ya timu kongwe kabisa ya Taifa hili, timu ya wananchi, timu yenye mataji mengi zaidi yaani mabingwa wa ki historia. Nikiwa kama shabiki wa Simba Sports Club basi sina la zaidi la kufanya ila kumpa mtani wangu Hongera ya kuongeza taji jengine kwenye historia yao na pia kumsifu round hii kwa kutuzuia kuchukua ubingwa kwa mara ya tano MFULULIZO.Engineer Hersi Ally Saidi aliingia pale kwa njia ya mdhamini (GSM) ila baada ya kuonekana kazi nzuri ambayo ameifanya kwa kipindi cha miaka miwili...2022-06-231h 29Salama NaSalama NaSE7EP01 - Salama Na ZUCHU | SINDANOKuna usemi mmoja unaenda kama hivi, kulea mimba si kazi ila kazi ni kulea mtoto, tafsiri yangu naamini mhenga hapo alikua anatuambia kazi pengine inaanza baada ya kupata kazi, tunaelewa jinsi gani ambavyo kupata kazi huwa ni kazi. Tena kazi yoyote, haijalishi kama ni ya upishi au ulinzi au ufundi au hata u daktari, mi nawajua madaktari kadhaa ambao nao pia wanapata shida kupata hizo kazi. Na baada ya kupata shida zote hizo wakati wa kutafuta kazi basi kazi halisi huanza pale unapoipata sasa hiyo kazi yenyewe. Kazi ya Zuchu ilianza kabla hajaipata hiyo kazi yenyewe na...2022-06-1655 minAdrián Salama ¡Sin Censura!Adrián Salama ¡Sin Censura!1364. Relación de controlEn el siguiente video el Dr. Adrián Salama habla acerca de cómo una relación puede cambiar de estar con alguien por amor, a estar con alguien por control, por sentir o creEn el siguiente video el Dr. Adrián Salama habla acerca de cómo una relación puede cambiar de estar con alguien por amor, a estar con alguien por control, por sentir o creer que tienes el control sobre la otra persona. Si esto esta pasando, mira el siguiente video. er que tienes el control sobre la otra persona. Si esto esta pasando, mira el sigui...2022-03-2310 minAdrián Salama ¡Sin Censura!Adrián Salama ¡Sin Censura!1242. Chantaje emocional en parejasEn el siguiente video el Dr. Adrián Salama habla acerca del chantaje emocional que es comúnmente utilizado en una relación tóxica, con el fin de lastimar a la otra persona para obtener algo que esa persona quiere. El Dr. Salama demuestra lo que es poner un límite claro ante el chantaje emocional. Si quieres saber más, mira el siguiente video.Support this show http://supporter.acast.com/adrian-salama-aqui-y-ahora. Hosted on Acast. See acast.com/privacy for more information.2021-12-1111 minAdrián Salama ¡Sin Censura!Adrián Salama ¡Sin Censura!1162. La ansiedad se vaEn el siguiente video el Dr. Adrián Salama apoya a una persona que está viviendo una época muy difícil en su vida. Sobre todo en esta época, la ansiedad está presente y el Dr. Adrián Salama habla de formas que pueden ayudarte para que salgas adelante y disminuir tu ansiedadSupport this show http://supporter.acast.com/adrian-salama-aqui-y-ahora. Hosted on Acast. See acast.com/privacy for more information.2021-10-3012 minAdrián Salama ¡Sin Censura!Adrián Salama ¡Sin Censura!Ainara Suárez rompe el silencio con el Dr. SalamaEste es un nuevo podcast llamado Vulnerable y espero te gusteSupport this show http://supporter.acast.com/adrian-salama-aqui-y-ahora. Hosted on Acast. See acast.com/privacy for more information.2021-10-071h 12Adrián Salama ¡Sin Censura!Adrián Salama ¡Sin Censura!Adrián Salama en el programa The Red FlamingoFui invitado a participar en este podcast con grandes chicas y esto fue lo que pasóSupport this show http://supporter.acast.com/adrian-salama-aqui-y-ahora. Hosted on Acast. See acast.com/privacy for more information.2021-05-2433 minSalama NaSalama NaEp. 55 - Salama Na PROFESA | MAPINDUZI HALISISALAMA NA PROF JAY --- Support this podcast: https://anchor.fm/yahstonetown/support2021-02-251h 27Salama NaSalama NaEp. 54 - Salama Na RAYVANNY | NDAGHASalama Na RayVannay --- Support this podcast: https://anchor.fm/yahstonetown/support2021-02-181h 14Salama NaSalama NaEp. 53 - Salama Na NANDY | MNOGESHAJIHuyu si moja ya marafiki zangu, as in si Mtu amable nafahamiana naye sana, ambaye nishawahi kukaa naye muda mrefu na kupiga story, au kusafiri naye au kuwa studio wakati anafanya mambo yake au namjua mzazi wake au mtu wake wa karibu kwenye familia yake ila nawajua watu ambao wanamfahamu kwa ukaribu na watu hao ndo ambao walinipa mimi mawazo ya kutaka kumfahamu vizuri binti huyu hodari wa ki Tanzania bila ya hata ya wao kujua. Baadhi ya Dada zangu walifahamiana naye kwenye kipindi cha msiba wa Marehemu Ruge Mutahaba, kipindi hiko kilikua cha masikitiko kwao na...2021-02-111h 04Salama NaSalama NaEp. 52 - Salama Na HAJI | ALIYE KUTWIKA NDIYE ATAKAYEKUTUAHaji Sunday Manara nlitaka kusema ni rafiki YANGU ila vacati navaza hilo nikakumbuka mmh, Haji Sunday Manara ni rafiki wa WATU WENGI hususan mashabiki wa klabu wangu pendwa na zaidi kwa watu ambao hawapendi hata mpira ila wanampenda tu jinsi anavyoseti mambo yake na anavyoigeuza sehemu yoyote aendayo kama sehemu yake ya kujitamba na kujitutumua na tofauti yake na WACHACHE ambao wanafanya kazi kama yake ni kwamba yeye anaweza KUYATEMBEA yale anayo YAONGEA. Mapenzi yangu kwake ni ya first class na namini hata yeye analifahamu hilo, huwa namtazama kwa kuvutiwa hasa kwababu ya anavyojibeba na kukiaminisha kile...2021-02-041h 23Salama NaSalama NaEp. 51 - Salama Na Babu Tale | JUGGLERHamis Tale Tale ni MWAMBA wa maisha yake na ya wale walomzunguka kwa miaka nenda miaka rudi na kutoka upande huu wa muandishi na mtangazaji ni heshima tu kwenda mbele. Kuna msemo mmoja wa Kiswahili kuhusu nyani ambaye unamkuta mjini. Ya kwamba anakua kashakwepa MISHALE ya kutosha kwahiyo unapomkuta town inabidi umpe heshima zake za kutosha. Kwa waasisi wa Bongo Flava jina lake kuwa juu pale na haiwezi kuwa kosa hata kidogo na kuna wasanii kibao ambao wana mshutumu kwa mambo mengi lakini kuna wale ambao hawawezi kumsahau maishani mwao kwa sababu ya mchango mkubwa ambao amewapa...2021-01-3047 minSalama NaSalama NaEp. 50 - Salama Na SUGU | UJIO WA UMRITurudi nyuma mwaka 1999 wakati nilipomaliza kidato cha nne kwahiyo nilikua sina mitkasi mingi zaidi ya kumkimbia Mama inapofika mchana ili niende kucheza zangu basketball pale Msasani kiwanja cha Pazi. Nlikua natokea zangu Mbagala Charambe nachukua zangu basi mappa Mbagala Rangi tatu then muunganisho unaendelea mpaka nafika zangu mazoezini, nilifanya urafiki na makonda na madereva weeengi kiasi kwamba nilikua ‘staff’ kwenye daladala nyingi, na huwezi kuamini nyingi pia nilikua nikiingia basi radio nlikua namiliki MIMI. Station gani tunaskiliza au tape gani tunaweka ili safari inoge na muziki. Nakumbuka jinsi ambavyo Sugu alikua anaikosha, anakosha nafsi yangu na ya abiria wote amba...2021-01-211h 10Salama NaSalama NaEp. 48 - Salama Na JK | MSOGA UNOMuda si mrefu iliopita nilirudi nyuma kidogo kwenye kumbukumbu ya mawasiliano ya kwanza kabisa kati yangu na moja wa wasaidizi wake Mheshimiwa Jakaya Mrisho wa Kikwete na hiyo ilinirudisha nyuma mpaka mwezi wa tatu mwaka 2020. Kama mtu mwengine yoyote hii ilikua ndoto tu ambayo kwa Rehema na Baraka za Allah ilibidi itimie. Kwa Baraka zake hizo mimi na wenzangu tunashkuru sana sana kwa kuweza kulikamilisha hili. Shukran za dhati ziende kwa Doris Mollel ambaye kwa msaada wa Sadam ‘Almando’ Sanare alinimbia Doris anaweza akatu unganisha na mmoja wa wasaidizi wake ili tuweze kuona kama tunaweza pata hii nafa...2021-01-071h 01Salama NaSalama NaEp. 47 - Salama Na JOTI | SIMPLY SPECIALSalama Na Joti --- Support this podcast: https://anchor.fm/yahstonetown/support2020-12-241h 19Salama NaSalama NaEp. 45 - Salama Na TAJI | TABASAMU LA SWAHIBAPia anafahamkika kama Master T, mwenye sauti yake tamu ya kumfanya mtu abadilishe mawazo na kufanya anachosema yeye, lafdhi nzuri ya maneno ya Kiswahili na Kiingereza na tabasamu zuri kabisa lililokaa mahala pake na hiyo ndo tofauti ya Taji Liundi na watangazaji pamoja na hata viongozi wa department mbali mbali kwenye vyombo vyetu vya habari vya ‘siku hizi’. Taji alibahatika kuzaliwa kwenye familia yenye uwezo kwa kiasi chake na malezi bora aliyapata kwa Baba yake ambaye muda mwingi alikua akisafiri nchi mbalimbali kutokana na kazi yake na hii pia ilimfanya ajengeke kwa kiasi flani, kuweza kujiamini, kuongea lung...2020-12-1149 minSalama NaSalama NaEp. 44 - Salama Na MWAKINYO | VITASA OVERLOADHassan Mwakinyo kwa Mama yake ni kama ni kama mkate kwa chai tu, lazima ulainike. Sentensi hii imeanzia hapa baada ya kufuatilia kwa makini na kuambiwa hasa ni kitu gani kinachomfanya Champez atake kuwa bora zaidi na zaidi, na kutaka kupata kile anachokipata kwa nguvu zaidi na zaidi kila siku kila asubuhi anapoenda kukimbia, au kila jioni anapokua gym au anapokua ulingoni, na amini kwamba Mama yake ndo anayemfanya atake kuwa bora siku zote ili aweze kumbadilishia maisha yake kwa uzuri. Champez Mwakinyo sio moto pekee kwenye familia yao na Kaka yake mkubwa alianza haya mambo ya...2020-12-0300 minSalama NaSalama NaEp. 43 - Salama Na MANTANA | MIPANGO BAABAKaribu kwenye Salama Na --- Support this podcast: https://anchor.fm/yahstonetown/support2020-11-2600 minSalama NaSalama NaEp. 42 - Salama Na EDO KUMWEMBE | MWENYE SHOKA HAKOSI KUNIEdward ‘Edo’ Kumwembe ni rafiki yangu wa si miaka mingi, pengine sita tu toka mara ya kwanza kukutana nae wakati wa uzinduzi wa kampuni moja ya kamari hapa nyumbani. Nakumbuka alikua akimtania sana Fid Q na jinsi ambavyo Fid alikua hamjibu Edo ndo ilikua inachekesha kabisa, wengi wetu tunafahamu Fid ana maneno mengi, ila mbele ya Edo huwa hana hata maneno kabisa. Tulicheka sana, na baada ya hapo tukaanza kufanya kazi pamoja kama Influencers kwenye hiyo kampuni, na baada ya miaka  mitatu Allah akabariki nikapata ile kazi ya Super Sport, na kama ulikua hufahamu, Edo ndo alinipigia chepuo nyin...2020-11-1900 minSalama NaSalama NaEp. 41 - Salama Na KALITO | THE ORIGINATORCarlos Bastos aka Kalito ni moja kati ya wale binadamu ambao hawahitaji ‘kutambulishwa’ na hiyo si kwa sababu ya muonekano wake hata kidogo zaidi ni personality yake, anaongea, anachekesha, anajielewa, anajua nini cha kusema na wapi pa kusema pia. Katika watu ambao namshukuru Mungu kwa kuwafanya wawe rafiki zangu Kalito ni mmoja wapo. Jinsi ambavyo alifika Tanzania inaweza ikakufanya ujue pia yeye ni mtu wa aina gani haswa, kutoka mwenyewe familia ambayo mtoto wa kiume ni pekee, na pengine alikua na uhakika wa kupata kila anachotaka lakini aliamua kupaki begi na kuchanja mbuga kuja hapa Tanzania. Kusema za u...2020-11-1200 minSalama NaSalama NaEp. 40 - Salama Na KADUGUDA | SIMBA WA YUDAMara ya kwanza kukutana na Mwina Kaduguda na tukaongea kiasi ilikua kwenye seminar ambayo timu ya Simba ya wanawake ilikua imeandaliwa kwaajili ya kuwaweka sawa kwenye masuala ya biashara, jinsi ya kujitunza wao na vipaji vyao, jinsi ya kuishi na umaarufu na pia kusimamia masuala yao ya kifedha. Mzee Kaduguda alikuwepo kwenye kikao hiko akiwa kama Mwenyekiti wa klabu ya Simba, na pia mmoja wa watoa nasaha kwa mabinti hao. Na kusema za ukweli toka siku hiyo baada ya kumsikiliza akiongea na wachezaji wale pamoja na Mimi ambaye nilikua mgeni tu kwenye seminar ile, nilivutiwa sana na...2020-11-0500 minSalama NaSalama NaEp. 39 - Salama Na DULLA | GO HARD OR GO HOME...Abdallah Khamis Ambua ndo jina halisi toka kwa wazazi wake ambao hawana asili ya kisiwani wala kuwahi kuishi huko kwa muda mrefu ambako pengine ndo kukamuwezesha kupata hiyo lafdhi. Kabla hatujafika kokote kwa kuskia kutoka kwangu, ningepeda ufahamu kwamba mimi si mmoja ya watu walotaka Dulla apewe kipindi cha Planet Bongo mwaka 2018 wakati naenda zangu Cardiff kushangaa kondoo, na moja ya sababu zangu kubwa ilikua yeye kutokua na lafdhi nzuri ya maneno kwenye lugha yetu adhimu ya Kiswahili. Na hilo nililiweka wazi haswa. Lakini pia nilikubaliana na matokeo baada ya viongozi kuamua kumpitisha yeye, na kwa heshima zote leo...2020-10-2200 minSalama NaSalama NaEp. 38 - Salama Na CHARLES HILLARY | MZEE WA BUSARAIlinichukua muda mrefu kuweza kupata nafasi ya kuongea uso kwa macho na Charles Hillary, maana toka enzi za Mkasi nilikua natafuta mwanya wa kuweza kukaa nae chini walau kwa hata nusu saa tu. Sikuwahi kukata tamaa badala yake nilikua kama chui kwenye mawindo yake, na mwisho wa siku kwa uwezo wa Mungu, binti yake Faith, Ivona Kamuntu na Mama kule nyumbani waliniwezesha kushinda mechi hii hatimaye. Mungu anajua tabasamu lilikua la ukubwa wa kiasi gani, na pengine hilo linaweza likawa limefanya niwe excited sana mpaka mengine nikayasahau kuyauliza, au kujua naulizaje, au kushangaa sana? Ushawahi kukutana na mtu alafu...2020-10-1500 minSalama NaSalama NaEp. 37 - Salama Na DR MWAKA | BINGWASikuwahi kukutana na Dr Mwaka mimi kabla ya tarehe 26 ya mwezi wa tisa, ila nilishawahi kuongea nae kwa simu mara mbili kabla ya kukutana, hatukuwa marafiki ila maongezi yetu ya mara ya kwanza kwenye simu yalinifanya nijue kwa kiasi yeye ni mtu wa aina gani, na nilivyokutana nae pia iliongeza heshima yangu kwake kwa kazi anayofanya na aina ya mtu yeye alivyo. Nisiseme kwa kupepesa, alini impress na nilijifunza vitu kadhaa kwa muda mchache niliokaa naye na kuongea nae. Alikuja na mkewe kwenye set ya kipindi na alihakikisha mkewe anafika mpaka kwenye ‘kizuizi’ cha mwisho kabisa kabla ya k...2020-10-0800 minSalama NaSalama NaEp. 36 - Salama Na JOH MAKINI | KIUNGOStory ya kwanza siku zote itakua ni jinsi ambavyo mimi na Joh Makini tulipokutana mara ya kwanza, nakumbuka vizuuuri sana sana haswa, jinsi alivyokua mwembamba na asiyekua na maneno mengi, ila macho yake, macho yake yalikua kama Askari wa shabaha ambaye akilenga hawezi kukosa, na guess what? Wanasema katika vitu ambavyo havibadiliki kwa binadamu anapokua basi macho ni moja wapo. Macho yake ni yale yale ya sniper, ila kwa sasa ni ya sniper aliye relax ambaye shabaha zake na malengo yake yanaeleweka. Hahitaji kujitambulisha anapokua kwenye mawindo yake. Heshima zangu nyinyi zinaenda kwake, maana kuweza kukaa kwenye...2020-10-0151 minSalama NaSalama NaEp. 35 - Salama Na KAJALA | JERAHA LA MOYOKajala Winfrida Masanja ndo jina lake alipopewa na Mama yake kipenzi alipozaliwa. Mama ambaye alikua akilitumikia jeshi la Polisi Tanzania miaka ya nyuma, ambaye alihakikisha binti yake huyu anakua katika maadili yaliyo bora na nidhamu yake iwe ya hali ya juu. So nini haswa kilitokea mpaka akawa si mtoto mzuri yule ambaye Mama alifanya kila aliwezalo kuhakikisha anakua hivyo miaka ya nyuma? Sasa ni Mama na mfanyabiashara anayejielewa tu. Ila yepi haswa ambayo yalishawahi kutokea kwenye maisha yake na ambayo hajivunii hata kidogo? Mimi na K tunafahamiana miaka mingi sana, mara ya kwanza tulikuna kwenye michezo, kwenye...2020-09-2456 minSalama NaSalama NaEp. 34 - Salama Na DOGO JANJA | YENTENakumbuka mara ya kwanza kukutana na Dongo Janja enzi hizo akiwa mtoto kabisa na hata kwenye viduara vyetu alikua anakaa mbali maana havikua vinamhusu. Kukua kwake kwenye macho yetu wakati mwengine inatufanya tuwe tunadhani kama tunamfahamu sana au tuna haki sana ya kujua kila kitu kwenye maisha yake na kumhukumu kwa maamuzi mengine ambayo sisi kama sisi hatujayapenda, tunasahau kama hayo ni maisha yake na ana haki ya kujifunza kwa kukosea na kukaa sawa kama ambavyo yuko sasa. Jina la serikali ni Abdulaziz Abubakar Chende aka JANJARO, sio DOGO JANJA tena, sasa ana miaka 25. Unakumbuka mara ya...2020-09-1748 minSalama NaSalama NaEp. 33 - Salama Na SPESHOZ | BOBBINJeffrey Jessey Mmbungu ni kijana wa ki Tanzania ambaye aliangaliaaa wapi pa kupata rizki ili mambo yake yamuendee kama anavyopenda na akafanikiwa kwa asilimia nyingi sana huku akipata pointi nyingi za kujiamini na kuthubutu kutoka kwangu. Ni rafiki yangu kwa miaka zaidi ya minne sasa, tunagombana tunapatana, kisha tunagombana tena alafu tunapatana, kisha tunagombana kwasababu ya Manchester United alafu tunapatana tena kabla hatujagombana tena kwasababu ya suit yangu kutotobolewa mashimo ya vifungo vya pembeni ya suruali yangu, au pengine kwasababu nlikua nataka kumpiga kirungu akachomoa, au pengine simu yake haipatikani kiiiila wakati wakati yeye ni mtu ambaye hatakiwi simu...2020-09-101h 23Salama NaSalama NaEp. 32 - Salama Na Riyama | UTAKWENDA UTARUDI Riyama Seleman Ally, malkia wa kazi aifanyayo na kila alitilialo msisitizo hulifanya kwa asilimia 100, hata kama akichelewa kama pengine alivyochelewa kupata heshima yake na malipo yake anayostahili, kama ambavyo anapata sasa au ambayo anapata maana safari bado ni ndefu. Na kwa mazungumzo haya nilofanya naye huo ndo muelekeo na ndo nia na madhumuni. Sote tunajua PENYE NIA PANA NJIA, so kazi ni kwetu. Mzaliwa wa Unguja Tanzania, kakua katika familia ya kidini na malezi bora ila kwa mujibu wa maongezi yetu haya yeye alipenda zaidi kuwa muimbaji, kitu ambacho Mwenyezi Mungu mtoa vipaji hakumjaalia kipaji hicho...2020-09-031h 15Salama NaSalama NaEp. 31 - Salama Na GOODLUCK | WASTAHILI SIFASifa za Bwana inabidi zisemwe kwa zawadi hii alotupa sisi wanadamu, tunamshkuru sana kwa kipaji cha Goodluck Gosbert na tunamshkuru pia kwa kumfanya ni wa kwetu, kutoka nchini kwetu, kwamba ni mwenzetu. Kwa kweli binafsi nimependa sana na najivunia yeye. Utamu wa sauti yake nadhani cha kwanza wengi tulikipenda sana, baada ya kumsikia tu, kama ilivyokua mara ya kwanza anataka kujifunza kupiga gitaa akaenda kanisani, na akaskika akiimba na wana kwaya wa kanisa hilo na wakampenda toka siku hiyo mpaka leo, ndo ilivyokua kwetu pia naamini. Kipaji chake cha pili ni utajiri wa mashairi, kipaji kikubwa cha...2020-08-271h 04Salama NaSalama NaEp. 30 - Salama Na SEVEN | ROCKSTARMtaani huwa wanasema ‘hizo kazi za wanaume’, maana mambo ya kukesha na watoto wa kiume na kuhangaika nao usiku na mchana kwa mwanamke inakua ngumu, na pengine inaweza ikaleta mambo yasiyohusu au ikasababisha vitu nyengine visiende kwasababu tu anayefanya hiyo kazi ni MWANAMKE. Ila kwa Christine ‘Seven’ Mosha nadhani hayo maneno yalikua ndo mafuta kwenye utambi wake na aliyatumia hayo kuweza kutoa mwanga maridhawa ulioset standard ya kuvutia. Kuna kipindi na mpaka sasa, ukiwataja ma meneja wa wasanii walio hodari hapa kwetu basi la Seven litakua la kwanza kwa mujibu wangu Mimi, maana kwa kuwa mfano kwenye tasnia aliweza haswa!2020-08-201h 07Salama NaSalama NaEp. 29 - Salama Na CPWAA | KILA CHOMBO CHA WIMBILEWakati Parklane iko juu sana wengi wetu tulikua tunamfahamu zaidi Sumalee na ilikua haswa Sumalee na yule mwengine mwenye sauti nzito ambaye alikua anatupia tu vichombezo vya hapa na pale, hata kwenye posters za show na mambo mengine Ismail Sadiq aka Sumalee ndo alikua kila kitu mpaka pale kundi lilipovunjika na kila mmoja akaenda upande wake, hapo ndio tulipoanza kufaidi kipaji cha huyu mwanachama mwengine wa hiyo duo, jina la serikali ni Ilunga Khalifa aka Cpwaa alianza kung’ara zaidi na kupata mpaka show za kimataifa.  Yuko na swagg, anaweza kuongea kiswahili na ki...2020-08-131h 04Salama NaSalama NaEp. 28 - Salama Na SHANGAZI | FIRST BORNFatma Abeid Amani Karume ni mtoto wa kwanza wa rais wa sita wa Zanzibar na pia ni mjukuu wa rais wa kwanza wa Zanzibar na kiongozi wa mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 na pia ni mwanasheria hodari, na siku za hivi karibuni amekua mstari wa mbeeele kupaza sauti kwenye masuala ya kisiasa hapa nyumbani Tanzania na ni kitu ambacho kimempa umaarufu mwingi kwa wananchi na kupachikwa jina la Shangazi, yeye ndo SHANGAZI wa Taifa. Kuzungumza naye imekua kama mtihani kiasi maana yeye ni wakili na sote tunafahamu jinsi ambavyo mawakili wanavyojua kuongea kwahiyo ilibidi nitulize nywele kweli...2020-08-061h 23Salama NaSalama NaEp. 27 - Salama Na SEBA | MKURUGENZISebastian Bigacho Ndege, jina kubwa  nchini kwetu na anajulikana na watu wa aina tofauti tofauti, hiyo ndo tofauti yake yeye na ‘celebrities’ wengine. Ukiachana na kwamba ni Daktari hodari tu na mtangazaji wa radio mahiri kabisa ambale alijenga historia miaka ya nyuma kwa kuwafanya watu wawe huru kuongelea juu ya suala la maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi, Seba (hivyo ndo anavyofahamika zaidi au Dr Seba au hata Jembe ni Jembe) aliweza kuwafanya watu wawe huru kuongelea pia masuala ya magonjwa ya zinaa na unyanyasaji wa kijinsia kwenye kipindi chake cha NJIA PANDA. Kutumia kipindi hiki, aliweza pia kubadilisha mais...2020-07-301h 19Salama NaSalama NaEp. 26 - Salama Na Baba Levo | ALL IN ALLKusema ukweli kabisa mimi na mgeni wetu wa wiki hii hatuna urafiki wala mazoea kabisa, ila tunafamiana kwa mbali na pengine (naamini) kila mmoja anamheshimu mwenzake kutokana na kazi ambazo kila mmoja wetu ameshafanya, na hiyo ndo ambayo imeleta heshima kati yetu. Pia tukumbuke heshima hainunuliwi wala haihongwi, huja yenyewe na kutuwama pale inapoona inafaa. Kwa kipaji na jina lake kuwa kule na huku nami ndo nilimfahamu Baba Levo. Utani wake kwa wasanii wengine (hasa siku za hivi karibuni) watanzania wamekua wakiuona sana. Ila kwa mujibu wa historia chache juu yake ambayo nilikua naifahamu Baba Levo siku...2020-07-231h 21Salama NaSalama NaEp. 25 - Salama Na Gabo | MTOGAPAAFWEJina halisi ni Salim Ahmed Issa, na kwa mujibu wa niloyasoma ni mjukuu wa moja ya watu maarufu mkoani Iringa ambaye alikua anatambulika kama Mtogapaafwe Kiyeyeu. Huyo alikua ni BABU wa Gabo Zigamba kabisaa ambaye binti yake Rafia Issa Kiyeyeu ndo Mama mzazi wa Gabo huyu tunayemfahamu mimi na wewe. Unaambiwa kaburi la Marehemu Mzee Mtogapaafwe lilikua na maajabu sana, ila hiyo ni khadithi ya siku nyengine. Hapa ilikua juu ya utambulisho wetu kwake na sifa zake actor hodari toka kwetu Tanzania. Gabo si moja ya marafiki zangu ila baada ya kuonana hapa ndo urafiki wetu ulipoanzia...2020-07-1652 minSalama NaSalama NaEp. 24 - Salama Na Lady Jaydee | POWERHOUSEKwa Judith Wambura Mbibo kuongea anayoyawaza bila ya kupepesa au kutafuta sapoti kabla hajafanya hivyo ndo hulka yake haswa, si wa kukwepeshakwepesha au kung’ata maneno ili yawe malaini zaidi kwa anayeambiwa asijikie vibaya labda. Kwake yeye lilivyo ndo lilivyo, kazi ya kupaka mawingu rangi huwaachia wahusika, yeye yake ni kuhakikisha mawingu yapo, na kwa hilo? Mimi namheshimu sana. Mwanangu mwengine ambaye hii ni mara yetu ya kwanza kukaa chini na kutia story ili wananchi waweze kupata majibu ya baadhi ya maswali waliyokua nayo muda mrefu sana pengine. Na round hii nilihakikisha sichezi mbali naye kama Chama na...2020-07-0957 minSalama NaSalama NaEp. 23 - Salama Na Nizar | RAHA LEO KUCHELEWakati Vancouver White Caps wanamtaka Nizar Khalfan baada ya kumuona akiwa anakipiga hapa nyumbani wakati yuko na timu ya Taifa ya Tanzania haikua habari au jambo la kushangaza miungoni mwa wachezaji na walokua wakimuona na kumfahamu mchezaji huyo vizuri. Kila mtu kati ya hao alikua akiomba ki vyake kijana huyu kutoka Kusini mwa Tanzania apate nafasi ya kwenda kuwakilisha Taifa na kuendeleza kipaji chake maridhawa kabisa. Nizar ametokea Mtwara na kwenye familia yake kwa mujibu wa maongezi yetu Mzee wake alikua akiupiga ingawa si mwingi kama wa Master Chef Khalfan maana yeye alianza akiwa mduchu haswa, watu wazima wa mtaani...2020-07-021h 25Salama NaSalama NaEp. 22 - Salama Na Isaya | KOMAA NAOMimi na Isaya mara ya kwanza tumekutana kwenye set wakati tunatengeneza episode hii ya 22 lakini kabla ya hapo ilikua ni kufahamiana tu kule kwa social media na respect kwa kila mmoja wetu kwa kile ambacho mwenzake anakifanya. Kwahiyo mkutano wetu wa kwanza ulikua ndo wa kwanza kabisa na haikua ngumu kuanzisha maongezi kati yetu. Wakati nishamseti ili aje kwenye meza pia niliwauliza wenzangu tunaofanya hii kazi pamoja, kila mmoja apendekeze jina au majina ya watu ambao wangependa waje kwenye kipindi na kila jina liwe na sababu ya kwanini tumpe nafasi huyo mtu. Basi jina lake pia lilikua...2020-06-2554 minSalama NaSalama NaEp. 21 - Salama Na Baraka | FAHARI TOKA ITETEMimi ni kama wewe tu juu ya ufahamu wa huyu mtu ambaye ameibeba Itete iliyopo kata ya Isuto tarafa ya Isangati, wilaya ya Mbeya vijijini mkoani Mbeya na Tanzania kwa ujumla, jina ni Baraka Adson Mpenja. Wengi humuita sauti ya radi, utamshi wake wa maneno na majina ya wachezaji na viongozi ni wa namna ya kipekee haswa, na bila ya shaka hiyo ndo tofauti kuuubwa kabisa kati yake yeye na watangazaji wengine wa kabumbu ikiwa pamoja na mimi hapa Tanzania. Ni kijana na ni maridadi na pia hajasahau wapi ametoka na ndoto zake ndo hizi ananoziishi sasa...2020-06-181h 29Salama NaSalama NaEp. 20 - Salama Na Lord Eyes | HAWATUWEZIIsaac ndo jinsi jina lake linavyoandikwa, kipaji adhimu kabisa kutoka Kaskazini mwa Tanzania, Allah kamjaalia kila ambalo msanii anaomba abarikiwe nalo wakati anapewa kipaji. Mrefu, muonekano mzuri, mashairi ya kibabe na kujiamini kulikokaa sehemu yake haswa. Walipoanza kama kundi hapo ndo attention yangu waliipata wana Nako 2 Nako Soldiers kutoka Ara, kila kitu kilikua tofauti juu yao, mavazi, style, matamshi na hata muonekano. Hii ilikua chachu ya kuwafikisha popote ambapo walikua wamepalenga. Mashabiki kila kona ya Tanzania na Afrika na dunia kwa ujumla, hakuna radio utakayoskilizia ambayo walikua hawapati nafasi. Walikua marafiki wa kila kituo na kazi yao...2020-06-1153 minSalama NaSalama NaEp. 19 - Salama Na Monalisa | MASHHURAKabla sijasema jinsi ambavyo nampenda na kumheshimu mgeni wetu wa wiki hii napenda kusema cha kwanza ambacho nilikipenda kwake kwanza ilikua jina lake, Ms Yvonne Cherrie kisha Monalisa. Rafiki mzuri, mstaarabu na mtu mwema sana. Mona pia ana bahati sana, bahati ya kuwa na Mama ambaye ni hodari na mcheshi ambaye nae alifanya kazi yake ya kuhakikisha bintiye kwanza anafanya yote anayostahili kufanya kama mtoto kabla haja mshika mwanaye mkono na kumtambulisha kwenye dunia ya sanaa ambayo ilitufanya tumtambue na kumpenda pia na pia kuwakubali zaidi kama Mama na mtoto ambao ni mahodari sana. Kwenye...2020-06-041h 00Salama NaSalama NaEp. 18 - Salama Na Madee | MPAKA MISHALEMara zote ukiwaza Manzese kama wewe ni mpenzi wa Bongo Flava basi utawaza Madee tu. Waliosema au alipojiita Rais wa kule sidhani kama kulikua na upinzani wowote, najua kulikua na mtu mwengine ambae alikua anataka hiyo title ila tayari ilikua na mwenyewe ambaye inamkaa haswa. Busara zake za miaka ya karibuni na haswa niseme zaidi mwaka huu ni moja ya vitu vilinivutia kutaka kuongea nae. Maana si mara nyingi kwa kijana ambaye amekulia maisha ya ‘ki gangster’ kuwaza watu wengine au hata kuonyesha kuguswa na kitu flani. Ili mtu afikie kufikiria suala la umri kwenda na kuanza kuji...2020-05-281h 08Salama NaSalama NaEp. 17 - Salama Na Shikana | DYNAMITEMi na rafiki yanyu huyu tumepishana zaidi ya miaka kumi na nne, wakati anazaliwa mimi nilikua nagombana na makondakta kupata nafasi kwenye chai maharagwe ya kutoka Buguruni kuelekea Posta. Ila kupishana kwetu kwa umri naamini ndo kunaufanya ushoga wetu uwe special zaidi, maana yeye akiwa ananikhadithia kinachokiki kwenye umri wake, nami nakua namuelezea challenges za unapozidi kukua na naamini hii inatufanya tuwe bora zaidi. Na ki ukweli mara nyingi yeye amekua shujaa wangu, maana kuna mengine mazito kwake yanakua mepesi tu na hunisaidia kuona mambo kwa picha tofauti. Kwa hilo namshukuru sana. Wakati mwengine wanasema umri sio kipimo cha...2020-05-2145 minSalama NaSalama NaEp. 16 - Salama Na Darassa | KAWIA UFIKEThabit Shariff Ramadhan my guy, siku zote mkimya, yupo kama hayupo, anayeona lakini humkuti anaangalia na mwenye kuyabeba yanayobebeka na kuyaacha ambayo hayapaswi kuchukuliwa, huyo ndo yeye na leo ukimuona mpe tu heshima zake, pengina si kwasababu kakuzidi umri, ila kwasababu aliyechelewa lakini KAFIKA. Tena, sikumbuki lini ilikua mara ya kwanza mi naye kukutana ila nakumbuka nilipomuona 2016 mwezi wa 12 kwenye mazoezi ya show ya usiku ya Tuzo za Muziki za EATV, alikua wa mootoh, ukiachana na watu waliokua ndani ya game, hakuna aliyejua alitokea wapi, ila boom!! Kwenye sikio na kila mdomo wa wana Afrika ya Mashariki...2020-05-1445 minSalama NaSalama NaEp. 15 - Salama Na Rosa Ree | OSHUNUkiwa zako nyumbani umejikalia kwenye sofa unamuangalia Rosaree kwenye TV kwa mara ya kwanza sidhani kama utaweza kugandua macho, pengine ukiwa na watu walokuzidi umri style yake inaweza ikawashtua kiasi na haswa wakiskia anachoimba ni kwa lugha ya Kiswahili ndo kabisa. Ki ufupi binti huyu toka kwenye familia yenye story ambayo kwa ki binadamu si tu yeye pekee amepitia, lakini ni yeye ambaye anafahamika na wengi kati yetu na hii ni nafasi yako na yangu pengine ya kutufanya tuamini kwamba ulichopitia au unachopitia, huko peke yako na pia hayo mambo yana mwisho wake. Ki kawaida Rosaree sio...2020-05-0742 minSalama NaSalama NaEp. 14 - Salama Na Romy Jones | PLUGRomeo boy handsome toka Kinondoni mpaka Tandale na sasa duniani kote. Ni kijana wa town, mcheshi, mtanashati, mwenye madevu na mcha Mungu, Ila pia ni Kaka yake mwanamuziki superstar toka Tanzania ambaye ni Diamond Platnumz. Mimi na Romy tunafahamiana miaka mingi, na kama ulivyodhani nilianza kumjua yeye kabla sijafahamiana na Nasib, story yetu inaenda toka enzi za ‘ujana’ wetu, rafiki zake ndo rafiki zangu na tulikua tukikutana karibia kila wiki. Toka Platnumz awe al maaruf Romy amekua nyuma yake siku zote, toka video ya kwanza ambayo umemtuambulisha kwetu super star huyu Romy alikuwemo pia kwenye vide...2020-04-3052 minSalama NaSalama NaEp. 13 - Salama Na Zuhura | DADAKEMoja ya watu walopigana vita zao wenyewe kimya kimya na wengine wakashuhudia tu mtu yuko jukwaa la kimataifa na anazidi kusoga. Maana halisi ya nitafanya kama ilivyo ili tuone mbele itakuaje maana Mungu amekua mwema haswa, so kwake yeye hakuna kinachoshindikana na kiukweli kabisa kama wewe ni wa mbili basi utaendelea kuzivaa maana mwenye hizo mbili kuvaa moja abadan! Mimi nilikutana naye kwa mara ya kwanza kwenye mahangaiko ya kazi yangu ya kwanza, radio mpya ilikua imeanzishwa hapa mjini, kwa msaada wa Soggy Doggy Anter aka Chief Rumanyika nikapata nafasi ya angalau kuingia mule ndani na nikakutana...2020-04-2354 minSalama NaSalama NaEp. 12 - Salama Na Gigy Money | ZILE KHADITHIMara nyingi huwa tunahukumu watu ambao hata hatuwafahamu na pengine hatujawahi hata kuongea nao hata mara moja kwasababu tu ya muonekano wao au kwa kitu tumeskia wamefanya au wamesema, au kwasababu fulani kasema jambo fulani kuhusu yeye ndo hapo nasi tunajifanya tunawajua sana na kutoa hukumu zetu juu yao, kama vile tunawafahamu sana au tunajua sababu ya yote ambayo tumeona au kuskia tu wamefanya au kusema. Hayo ndo maisha ambayo mgeni wetu wa wiki hii amekua akiishi kwa miaka kadhaa sasa. Jina lake ni Zawadi aka Gift, binafsi sikumbuki siku ya kwanza kukutana naye au kumsikia ila...2020-04-161h 01Salama NaSalama NaEp. 11 - Salama Na Ben Pol | WA MNYANG’ANGAKatika pita pita zanguangu kwenye mitandao leo asubuhi nilikutana na video ya Ben Pol akiwa anaelekea kupanda zake helicopter na video ikamuonyesha akiwa anazunguka kwenye fukwe za huko alipokua na baadae ikaishia kwa kuonyesha watu wawili wakiwa wanaelea hewani... Mmoja wapo bila ya shaka alikua ni yeye, kuna mtu ambae amekua aki enjoy maisha yake miaka ya hivi karibuni kama yeye? Niko hapa nangoja jibu lako...  na bila ya shaka mmoja wa watu hao wawili alikua ni yeye. Kutoogopa na kutimiza malengo aliyojiwekea ndo siri ya kukamilisha hesabu alizokua kapiga, na bila ya shaka baraka za Mwenyezi Mungu...2020-04-0954 minSalama NaSalama NaEp. 10 - Salama Na MwanaFA | KARAMAWeekend mbili zilitopita rafiki yangu Mwinyi aka Mpwa aka Cousin aka Hamis alikua akiadhimisha siku ya kuzaliwa kwake na alikua amefiksha umri wa kustahili kusherehekea kwa kweli na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa maisha, mke wake kipenzi alinipigia simu siku nne kabla ya birthday ya mumewe na kutaka tujumuike nae kum suprise, pia akaniambia ana kazi sana ya kuweza kukamilisha hilo tukio maana jamaa (Mwana FA) kashasema yeye hana mango wa kutaka shughuli, angependa maisha yaendelee tu kama kawaida. Pengine alikua akitarajia dinner nyumbani na mkewe na wanawe basi. So kukawa na zoezi hapo la kuhakikisha jamaa hasomi mchongo na...2020-04-0255 minSalama NaSalama NaEp. 9 - Salama Na Khadija Kopa | ALIYEPEWA KAPEWAKhadija Omar Kopa.  Malkia wa mipasho na lejendari wa muziki wa Taarab kwenye ukanda huu na duniani kwa ujumla, mwenyewe kaniambia yeye kwenda Arabuni na Ulaya ni jambo la kawaida tu kwake maana hayo kayaanza kuyafanya kitaaambo sana. Kitambo kweli naweza sema, mimi nimeanza kumfahamu Da Khadija toka kigori kabisa, na amekua hapo kwenye standard hiyo hiyo kwa miaka nenda na miaka rudi. Hii bila ya shaka imetokana na kwamba na yeye alianza kufanya hizo kazi akiwa bado msichana mbichi kabisa. Na ameweza kutuliza akili yake na ku maintain standard na status yake kwa miaka nenda...2020-03-2650 minSalama NaSalama NaEp. 8 - Salama Na Idris | TROOPERMimi kama watanzania wengi sikuwa namfahamu Idris, mara yangu ya kwanza kumuona ilikua kwenye TV akiwa mmoja wa wawakilishi wa Taifa hili kwenye kipindi cha Big Brother mwaka 2014. Nilivyouandika hapa huo mwaka ndo imenigusa akilini kwamba ni miaka sita tu imepita toka Idris Sultan amekua kwenye macho na midomo yetu. Na pengine ataendelea kuwepo kwenye midomo na macho yetu kwa miaka mingi zaidi, kuna sehemu nilikua naangalia interview yake moja na alisema yeye umaarufu ndo kitu ambacho anakipenda zaidi, pengine na ndo maana alienda kwenye shindano la Big Brother Africa na toka ametoka mule kama mshindi sidhani kama kuna...2020-03-191h 01Salama NaSalama NaEp. 7 - Salama Na Fid Q | NGOSHA WA MBASANakumbuka kipindi ambacho Fidi alikua anaamini kabisa kama kuweka ‘uso wa mbuzi’ ndo kulikua kunakufanya uwe ‘hard core’, sina uhakika lini aliachana na dhana hiyo ila kwa kipindi cha miaka miwili au zaidi tabasamu na bashasha vimekua havibanduki kwenye uso wake, jambo ambalo mimi kama rafiki nalifurahia sana. Nakumbuka baadhi ya marafiki zangu wa kike ambao ni wapenzi haswa wa mziki wake walikua wakiniambia eh, sema rafiki yako mgumu jamani, Kha! Mi hucheka tu na baadae wakishazoeana basi sidhani kama kuna hata mmoja anaweza kusema kitu kibaya kuhusu yeye. Nilikua nacheka kwasababu mimi naamini namfahamu rafiki yangu huyu, yeye hupenda...2020-03-121h 23Salama NaSalama NaEp. 6 - Salama Na MxCarter | LENSMANLENSMAN Touch yake katika mambo mengi ndo ambayo inamfanya awe tofauti sana na vijana wengine walokuja mjini nae kwa wakati mmoja, uzuri ni kwamba nilikuwepo wakati mabegi (kama yalikuwepo) hata hayajatua uzuri chini ndo hapo nilikutana na Mashala, aka Michael Sylvester ‘Carter’ Mlingwa. Kwanza ilikua kujuana kwa kwenye mitandao tu na hiyo ni khadithi ya siku nyengine. Kwa wanao nifahamu mimi wanajua kama ni ngumu haswa kumuingiza mtu katika maisha yangu, awe karibu yangu, ajue undani wangu ndo maana nina watu wengi ninaofahamiana nao ila wanaonijua ni wachache. Michael ni mmoja ya watu wanaonijua mimi, na naweza kusema nami namj...2020-03-091h 07Salama NaSalama NaEp. 5 - Salama Na Shilole | MAMAZuwena Yusuf Mohammed ndo jina alopewa na wazazi wake na siko hapa kuwakosoa kwa chaguo lao hilo ila mi nadhani Shilole ndo limekaa mahala pake zaidi. Anaongea kama Shilole, anacheka kama Shilole, ni shujaa kama Shilole, REAL kama Shilole, anapenda kama Shilole na sisi tunampenda kama Shilole. Ally Rehmtullah alikua anaadhimisha miaka kumi ya kazi yake. So alifanya auditions kwa ajili ya kuchagua models kuelekea kwenye adhimisho lenyewe, Shilole aka Shishi alikua mmoja wa ma judge wa skuihiyo, picha likaanza hakuwepo popote pa kuweza kuonekana, shuguli ambayo ilichelewa kuanza kutokana na mambo mengine ilibidi pia iendelee bila yeye. Akatokea...2020-03-011h 11Salama NaSalama NaEp. 4 - Salama Na Barnaba | FUNDIBarnaba ni mfupi (siko hapa kumtoa kasoro) ila wazungu wana usemi wao ambao nitausema kwa kiswahili, ya kwamba vitu vizuuuri huja kwenye pakeji ndogo. Ukitaka kuelewa maana yake kama hujang’amua basi kamuulize Bibi. Umbo lake na uwezo havifanani , na kama ingekua ubora na kipaji ndo ukubwa wa mwili basi mwenzetu angekua kama HERCULES, pia siko hapa kwaajili ya kumtukuza bali kusema vile nimunavyo katika macho yangu. Ni kijana ambaye anajifunza kila siku iendayo kwa Mungu, hajawahi kujikweza, mwenye roho ya Imani, mwenye kumuogopa Mungu na pia asiyesahau alipotoka na pia alotoka nao huko alipotoka. Mtanashati pia, na...2020-02-241h 03Salama NaSalama NaEp. 3 - Salama Na Jokate | KAMISHNAMaana halisi ya ’nyota njema huonekana alfajiri’, najua sikuwepo hiyo ‘alfajiri’ wakati Mh Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe anazaliwa lakini hakika nilikuwepo wakati anamaliza wa pili kwenye mashindano ya Miss Tanzania mwaka 2006. Nilikuwepo pia kushuhudia jinsi alivyokua anapangua mikuki na mishale iliyokua inarushwa upande wake kwa zaidi ya miaka kumi na mitatu kabla hajapata cheo alichonacho sasa. Jokate amekua muerevu toka siku ya kwanza na kwa mazungumzo haya nilifanya naye bila ya shaka yatakupa mwangaza zaidi juu ya haya niyasemayo. Focus alokua naweka kwenye kila afanyalo ni funzo tosha kwetu sote na maana halisi hasa ya adui wa ndoto...2020-02-171h 08Salama NaSalama NaEp. 2 - Salama Na Marco Chali | DOKTADOKTA Marco na mimi tumekua marafiki wa miaka mingi na moja kati ya vitu vimetufanya tuwe marafiki ni kufanana kwetu kwa kupenda vitu vya aina moja. Kuanzia teknolojia mpaka muziki, nakumbuka siku ya kwanza kukutana naye, ilikua ni uzinduzi wa kipindi cha Bongo Star Search ambao ulifanyika Much More pale juu, alinifuata akaniambia juu ya mapenzi yake ya kipindi changu cha Planet Bongo enzi hizo na baada ya hapo ikawa ni urafiki ulodumu mpaka leo. Kipindi changu cha Mkasi kilizaliwa kwenye kibaraza cha studio kwa Marco Chali pale MJ RECORDS ambako ilikua ni maskani yetu kubwa mimi na...2020-02-091h 03Salama NaSalama NaEp. 1 - Salama Na Lil Ommy | AIR TABORA2016 ndo mwaka nilikutana na Lil Ommy mara ya kwanza, pengine nilishawahi kukutana naye huko nyumba ila sikumbuki. Aliniomba niende kwenye kipindi chake cha The Playlist enzi hizo kikiwa Jumamosi asubuhi ya tarehe 20 mwezi wa nane. Sikuwahi kupenda kufanyiwa interview ila siku hiyo nilimpa Ommy nafasi, sikuwahi kujutia na pengine hiyo ndo sababu ya kumfanya yeye awe mgeni nambari moja kwenye Podcast hii. Anayejitambua, anayejituma, anayesoma, mwenye nia na mipango endelevu… Nilimuomba aje na hapa tulizungumza karibia yote. Ya kwao Tabora, familia yao, marehemu Mzee wake, marehemu Dada yake, ndugu zake wa kambo, utundu wa udogoni, kutafuta kazi, maisha ya mj...2020-01-301h 07Adrian Salama aqui y ahoraAdrian Salama aqui y ahoraUn árbol que camina ep 22Nada te detiene hoy para ser la persona que deseas Desarrollar tus emociones es la clave para una vida de armonía y felicidad. Esta vida se traduce a éxito y abundancia. El resultado es tu libertad Este podcast está diseñado para hablar de los temas que sé que te pueden apoyar, así como las experiencias, conferencias y talleres en los que me he entrenado. Vamos a conectarnos Facebook.com/adriansalamaoficial instagram.com/adriansalama www.adriansalama.com Podcast para escuchar www.anchor.fm/adriansalama http://mx.ivoox.com/es/escuchar-adrian-salama_nq_364983_1.html O desde cualquier APP para escuchar podcast sólo p...2018-07-2000 minAdrian Salama aqui y ahoraAdrian Salama aqui y ahoraRazones para el divorcio ep 21Razones para dejar el amor hay varias, pero estas son las más escuchadas por un terapeuta amigo de ustedes. Desarrollar tus emociones es la clave para una vida de armonía y felicidad. Esta vida se traduce a éxito y abundancia. El resultado es tu libertad Este podcast está diseñado para hablar de los temas que sé que te pueden apoyar, así como las experiencias, conferencias y talleres en los que me he entrenado. Vamos a conectarnos Facebook.com/adriansalamaoficial instagram.com/adriansalama www.adriansalama.com Podcast para escuchar www.anchor.fm/adriansalama http://mx.ivoox.com/es/escucha...2018-06-2900 min